Hizi ni stahiki azipatazo mwajiriwa kutokana na mkataba wake wa ajira kukatishwa na mwajiri. Stahiki hizi hulipwa na mwajiri. kipengele cha 44 cha Sheria ya Kazi na Mahusiano Kazini Namba 6 ya mwaka 2004 inampa mwajiriwa haki ya kulipwa stahiki mbalimbali pindi mkataba wake wa kazi unapokatishwa.