Mfanyakazi anastahili likizo ya uzazi kama ifuatavyo:- a) Siku 84 za likizo ya uzazi yenye malipo iwapo amejifungua mtoto mmoja. b) Siku 100 za likizo ya uzazi yenye malipo iwapo amejifungua watoto mapacha c) Siku 84 za ziada za likizo ya uzazi yenye malipo ndani ya mzunguko wa likizo yake, iwapo mtoto wake atafariki ndani ya mwaka mmoja wa kuzaliwa na mfanyakazi huyo atapata ujauzito na kujifungua kabla ya miezi 36 kupita