Mfanyakazi anayestahili likizo ni yule ambaye tayari ameshafanya kazi kwa muda wa mwaka mmoja. Kwa mwajiriwa wa msimu (kipindi kifupi)ikiwa amefanya kazi kwa mwajiri huyo huyo kwa zaidi ya mara moja kwa mwaka na ikiwa vipindi hivyo alivyofanya kazi vinazidi miezi 6 na kundelea katika mwaka huo, basi anastahili likizo yenye malipo.