Halmashauri ya kijiji inapaswa kwanza kuwa na cheti cha ardhi ya kijiji ambacho, pamoja na mambo mengine kitaonyesha mipaka na ukubwa wa ardhi ya kijiji husika. Baada ya hapo kijiji, kikishajiwekea mpango wa matumizi bora ya ardhi na kutenga maeneo mbalimbali kwa shughuli tofauti, kinaweza kugawa hati miliki kulingana na matumizi yaliyopangwa kwa kila eneo