Kuna aina kuu mbili za Hati Miliki. Hizi hujumuisha Hati Miliki ya kimila ambayo hutolewa kwa mtu ambaye tayari anamiliki ardhi kwa njia ya kurithi bila maandishi yoyote, na hati miliki inayotolewa na kamishina baada ya kuombwa, hususan katika maeneo ya mijini. Lakini pia mtu anaweza kupata hati miliki kwa matumizi ya uwekezaji, kama vile mashamba makubwa, viwanda, nk