Mtu yeyote ambaye ni Mtanzania anaweza kumiliki ardhi mahali popote Tanzania Bara. Kwa Tanzania Zanzibar, haki hii imetengwa kwa ajili ya wazanazibari pekee. Lakini pia, Kikundi cha watu ambao ni raia wa Tanzania walio katika umoja unaotambulika au ni wabia au washirika, wanaweza kumiliki ardhi.