-kumwachia huru mshitakiwa kwa kutokuwa na hatia, pale upande wa mashitaka unaposhindwa kuthibitisha mashitaka na utetezi wa mshitakiwa kukanusha mashitaka hayo. -kumtia hatiani mtuhumiwa na kumhukumu kutumikia adhabu, kama upande wa mashitaka utathibitisha mashitaka dhidi ya mshitakiwa pasipo shaka yoyote na utetezi wake kushindwa kukanusha mashitaka hayo.