-Uhakika wa mtuhumiwa kufika mahakamani sikuatakayotakiwa kufanya hivyo. Katika kujiridhishana kigezo hiki, askari polisi huzingatia yafuatayo; -Historia ya maisha ya mtuhumiwa na mahusianoyake na jamii au, ajira yake -hali ya familia yake, na -Kumbukumbu/rekodi au habari za maisha yaketoka kwa polisi. -Mazingira ya kosa au tuhuma. -Maslahi ya mtuhumiwa, yaani Kipindi atakapotakiwa kukaa mahabusu kamadhamana itakataliwa ikiwa ni pamoja namazingira ya mahabusu penyewe, -Mahitaji au haja ya mtuhumiwa kuwa nje kwalengo la kuandaa utetezi wake au kufika kwakemahakamani, ikiwa ni pamoja na kupata ushauriwa kisheria na uwakilishi mahakamani, -Mahitaji ya kiusalama ya mtuhumiwa ambayoyanaweza kutokana na ulevi wa kupindukia,majeraha au matumizi ya madawa ya kulevya, -Usalama wa jamii hasa uwezekano wa mtuhumiwakuharibu ushahidi kwa kuwatisha mashahidi aukuwazuia polisi kufanya upelelezi.