Ikiwa mtuhumiwa anayehojiwa ni mtoto, afisa wa polisi mpelelezi (mfawidhi) anayemhoji mtoto huyo aliye chini ya uangalizi wa polisi, atawajibika kuwataarifu wazazi ama ndugu wa mtoto huyo kwamba, mtoto husika yupo kituo cha polisi kwa tuhuma ambazo ametuhumiwa nazo na yupo kwa mahojiano juu ya tuhuma hizo.