Sheria inampa haki polisi mpelelezi anayemhoji mtuhumiwa, kumzuia mtuhumiwa kuwasiliana na mwanasheria wake au ndugu zake, kama anaamini kwamba mawasiliano hayo yanalenga kusaidia kutoroka kwa mtuhumiwa mwenza, endapo tuhuma zinamhusu mtuhumiwa zaidi ya mmoja au ikiwa mawasiliano hayo yanaweza kupelekea kupotea au kuharibiwa kwa ushahidi wowote ambao unaweza kujumuishwa katika shitaka dhidi ya mtuhumiwa anayehojiwa.