Mtuhumiwa kabla ya kuhojiwa anapokuwa kituo cha polisi, anapaswa kuelezwa haki zake na afisa upelelezi anayemhoji lazima amwambie jina na cheo chake, mahojiano yanapaswa kufanyika katika lugha amabayo mtuhumiwa anaielewa vyema na pia mtuhumiwa asihojiwe mpaka awe amepewa tahadhari kwamba, hawajibiki kujibu maswali atakayoulizwa na afisa wa polisi mpelelezi na pia anayo haki ya kuwasiliana na mwanansheria wake ili awepo katika mahojiano hayo.