-Kupata utambulisho kutoka kwa askari polisianayefanya mahojiano. Hii ni pamoja na kuelezeajina, cheo chake na sababu za kutiwa nguvuni. -Kuelezwa kwa lugha fasaha inayoeleweka kwamtuhumiwa. -Kupata tahadhari kutoka kwa askari polisi anayehojikwamba hawajibiki kujibu maswali yote isipokuwayale yanayohusu maelezo binafsi (wasifu wake) najina lake. Hivyo mtuhumiwa ana haki ya kutojibu. -Kuwasiliana na mwanasheria wake au ndugu zakeakiwa mikononi mwa polisi, isipokuwa kama kunasababu ya msingi ya kuzuiliwa asiwasiliane na haowahusika. -Kuthaminiwa utu wake pamoja na haki zake zabinadamu. -Kupatiwa matibabu anapokuwa yu mgonjwa auamejeruhiwa katika hatua za ukamataji.