Kiutaratibu, mahojiano hufanyika kwa mdomo nakunakiliwa kimaandishi, na baada ya mahojiano mtoamaelezo anapaswa kutia sahihi yake kwenye maelezohayo baada ya kuridhika na usahihi wa maelezo aliyotoa. Endapo maelezo yaliyotelewa yanaendana na kutendekakwa kosa basi maelezo hayo pamoja na mtoa maelezoyatatumika katika ushahidi upande wa mashitaka pindishauri hilo litakapofikishwa mahakamani.