-Kuwepona hati ya upekuzi. -Kufanyika kwa upekuzi bila hati ya upekuzipale ambapo sheria inatoa mwanya kutokana namazingira. Kwa mfano, mtuhumiwa kuaminikakuwa ana silaha au kitu chochote kinachohatarishausalama na amani kwa umma. -Kufanyika kwa upekuzi nyakati za mchana yaanikati ya jua kucha na kupwa (kati ya mawio namachweo). Hata hivyo upekuzi unaweza kufanyikamuda mwingine wowote kama mahakama imetoaidhini ya kufanya hivyo. -Kufanyika kwa upekuzi mbele ya mashahidi ambaowanaweza kuwa: kiongozi wa mtaa au shina au mtumzima yeyote mwenye akili timamu. -Kama itatokea kuna vitu au mali imechukuliwakwa ajili ya ushahidi, basi ni lazima iandikishwe namhusika au mwenye mali kutia sahihi kuthibitishakutwaliwa kwa mali hizo. -Kutunzwa katika sehemu salama vitu au malizilizochukuliwa kabla ya kurejeshwa kwa mmilikihalali.