-kila mtuhumiwa ana haki ya kuthaminiwa utu naheshima yake au kutoteswa pale anapotiwa nguvuni -kila mtuhumiwa ana haki ya kuelezwa kosaalilotenda kabla ya kukamatwa. -kila mtuhumiwa ana haki ya kupewa ushauri wakisheria. -Ana haki ya matibabu pale anapokuwa ameumizwaau anaumwa. -Ana haki ya chakula na malazi. -Ana haki ya kuwasiliana na ndugu zake. -kila mtuhumiwa ana haki ya kukaa kimya mpakapale anapo hitaji huduma ya kuwakilishwa. -kila mtuhumiwa ana haki ya kupata dhamanaisipokuwa kwa makosa yasiyokuwa na dhamana. -kila mtuhumiwa ana haki ya kuyafahamu mashitakayake. -kila mtuhumiwa anahesabiwa kuwa hana hatia hadihapo chombo chenye mamlaka (mahakama) yakuzisikiliza tuhuma kitakapomsikiliza na kumuonana hatia dhidi ya kosa analotuhumiwa. -Kila mtuhumuwa atachukuliwa kuwa mwenye akilitimamu katika sheria ya makosa ya jinai hadi hapoitakapothibitishwa vinginevyo mbele ya sheria.