Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 inalinda haki za kiuchumi. Haki za kiuchumi ni pamoja na haki ya kufanya kazi na usawa katika sehemu za kazi. Haki hii imeainishwa katika ibara ya 22 ya Katiba. Na Ibara ya 23 imetoa haki ya kupata ujira na malipo ya haki kulingana na kazi ambayo mtu ameifanya.