-Lazima kuwepo na sheria inayoainisha kwa uwazi kwamba matendo flani yanapofanywa na watu kuwa ni jinai. -Sheria hiyo lazima pia ianishe adhabu kwa matendo hayo ambayo ni makosa ya jinai. -Wajibu wa kuthibitisha shitaka dhidi ya mshitakiwa ni wa yule anyelalamika, na kwa Tanzania ni Jamhuri, hivyo upande wa mashitaka unapaswa kuthibitisha shitaka lake dhidi ya mshitakiwa pasipo kuacha shaka. -Mtuhumiwa atachukuliwa kuwa hana hatia mpaka itakapodhibitika hivyo. -Mtu yoyote hatapelekwa gerezani pasipo kufikishwa kwanza Mahakamani.