Inapotokea msimamizi wa mirathi amekataa kutimiza wajibu huo, mmoja kati ya warithi au mtu yeyote mwenye maslahi kwenye mirathi ya marehemu anaweza kuomba mahakama imuite msimamizi huyo kujibu sababu za kutokutimiza majukumu hayo au imvue msimamizi huyo majukumu hayo na kumpa mtu mwingine aliye tayari kuyatekeleza majukumu hayo.