Msimamizi wa mirathi wa marehemu huyo anawajibika kuomba mahakama ya Tanzania kumtambua kama msimamizi wa mirathi hio. Maombi hayo huambatanishwa na kibali cha usimamizi wa mirathi kilichotolewa na mahakama ya nchi ambayo marehemu alikua raia wake. Taratibu hii hukubalika na kufuatwa na nchi zilizo katika jumuiya ya madola ikiwemo Tanzania.