Wosia ni kauli inayotolewa na muusia wakati wa uhai wake kuonyesha jinsi gani angependa mali yake igawanywe. Kwa maelezo hayo, mwili wa marehemu sio sehemu ya mali zake na hivyo wosia hauwezi kutumika kutoa maelekezo ya jinsi marehemu angependa kuzikwa. Marehemu atazikwa kwa mujibu wa mila, desturi au dini yake.