Sheria ya urithi na usimamizi wa mirathi imebainisha jinsi ambavyo madeni ya marehemu yanatakiwa kulipwa kwa kutoa kipaumbele kama ifuatavyo Kwanza- Gharama za mazishi na matibabu.Pili- Gharama za ufunguzi na usimamizi wa shauri la mirathi zikiwemo gharama za kuendesha shauri hilo.Tatu- Malipo kwa huduma zilizotolewa kwa marehemu na mfanyakazi, kibarua au mtumishi wa nyumbani.Nne- Malipo kwa madeni mengine yaliyoachwa na marehemu.