Mahakama inao wajibu wa kuchunguza kwa makini na kujiridhisha kwamba mtu anayeomba kuthibitishwa au kuteuliwa kuwa mtekelezaji au msimamizi wa mirathi, anayo maslahi katika mirathi hiyo na ataweza kufanya kazi hiyo kwa makini na uaminifu mkubwa kulingana na matakwa ya marehemu (kama yanaweza kubainika) katika kusimamia mali hizo.