Sheria ya ardhi ya vijijini namba 5 ya mwaka 1999 imesahihisha utaratibu wa umiliki ardhi wa kimila (urithi wa ardhi) kwa kuondoa ubaguzi wa aina yoyote kwenye umiliki wa ardhi na kuweka usawa kwa wanawake na wanaume. Kwa misingi hii, cheo cha tatu cha urithi kwenye sheria za kimila kinakua batili pale urithi wa mali ya marehemu unapogusia suala la ardhi.