Sheria ya Ardhi ya Vijijini (Namba 5 ya mwaka 1999) imesahihisha utaratibu wa umiliki ardhi wa kimila (urithi wa ardhi) kwa kuondoa ubaguzi wa aina yoyote kwenye umiliki wa ardhi na kuweka usawa kwa wanawake na wanaume. Kwa msingi huu, cheo cha tatu cha urithi kwenye sheria za kimila kinakuwa batili pale urithi wa mali ya marehemu unapohusisha suala la ardhi.