Sheria ya kimila katika tangazo la serikali namba 436 la mwaka 1963 haimruhusu mjane kurithi mali za marehemu mume wake. Mjane mwenye watoto inabidi aishi kwa kutegemea watoto wake. Mjane ambaye hana watoto atabaki katika nyumba ya marehemu na kupewa asilimia 20 ya nusu ya mali ya marehemu na kuitumia wakati wa uhai wake, akifariki au akiolewa na mtu mwingine nje ya ukoo wa marehemu mali hiyo na nyumba aliyokua anakaa hugawiwa kwa warithi halali wa marehemu mume wake.