Yapo mazingira ya aina mbili yanayoweza kuamua ni sheria gani itumike; Kwanza, pale ambapo mtu amefariki akiwa ameacha wosia, kile kilichoandikwa katika wosia ndicho kitakachoongoza mgawanyo wa mali na madeni yake, isipikuwa kama mahakama itashawishiwa kuamini vinginevyo. Pili, pale ambapo mtu amefariki bila kuandika wosia, kwa kuzingatia aina ya maisha aliyokuwa anaishi, mirathi yake itashughulikiwa kwa namna hiyo. Kwa mfano, kama marehemu aliishi kwa utamaduni na taratibu za kiislam, Sheria ya Kiislam kuhusu Mirathi itatumika.