Kama itagundulika kuwa mahakama imepokea na kutumia ushahidi flani kimakosa basi italazimika shauri hilo kurudiwa. Ili shauri hilo lirudiwe lazima kwanza idhihirike kwamba kuwepo kwa ushahidi huo kumepelekea maamuzi hayo yaliyotokea na kama ushahidi huo hauwezi kuathiri maamuzi ya mwanzo basi shauri hilo halitarudiwa.