Ndiyo. Kauli ya mwisho ya marehemu inaweza ikawa kwa njia ya mazungumzo baina yake na mtu wa mwisho kuwa nae (shahidi), ambapo mazungumzo yao yanapaswa kutolewa kama yalivyo. Kama kulikuwa na majibizano baina yao basi majibizano hayo yanatakiwa yatolewe kama ilvyotokea ili kupima uzito wa kauli zao kabla ya kutumia kama ushahidi.