Kitu kikubwa na muhimu kinachozingatiwa katika kauli ya mwisho ya marehemu ni taarifa juu ya chanzo na sababu za kifo chake. Kama kauli ya mwisho ya marehemu hailengi kutoa mwangaza juu ya chanzo cha kifo chake basi kauli hiyo haifai kuwa ushaidi katika shauri hilo.