Hapana. Ili jambo flani la kusikika likubalike kutumika mahakamani kama ushahidi ni lazima, kusiwe na ushahidi mwingine (bora zaidi) juu ya jambo hilo, shahidi aapishwe kabla ya kutoa ushahidi huo na lazima shahidi ahojiwe kwa kina na pande zote juu ya ushahidi anaoutoa.