Kuachishwa kazi isivyo halali ni pale ambapo mwajiri atashindwa kuthibitisha uhalali wa kumuachisha kazi mfanyakazi, au kutokuwa na sababu za msingi zinazoendana na matendo, utendaji na/au uwezo wa mfanyakazi, na hujumuisha pia kushindwa kuthibitisha kuwa kuachishwa kazi kwa mfanyakazi kulikuwa sahihi kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.