Ndiyo. Ni nyingi. Miongoni mwa hizo ni: a) Kupata uwakilishi pindi unapotokea mgogoro wa kimaslahi kazini baina ya mwajiri na mfanyakazi. b) Kutetea haki za wafanyakazi zisipindishwe na mwajiri , kwa mfano; haki ya likizo, mafao bora, nk c) Kwa niaba ya wafanyakazi, kuhamasisha waajiri kuweka mazingira bora, salama na yenye staha kazini. d) Kuwaelimisha wanachama wao juu ya haki zao za kazi, na namna bora ya kuzidai haki hizo.