huu ni mfumo wa kodi ambapo watu binafsi wasiokuwa na uwezo wa kutunza na kutengeneza hesabu za biashara hutozwa kodi kulingana na makisio ya mauzo ya mwaka. Na mlipa kodi alie katika mfumo huu hatakiwi na sheria za kodi ya mapato kuandaa na kutuma hesabu za ukaguzi mamlaka ya mapato (TRA).