Sheria za kodi zinatoa misamaha mbali mbali kwa biashara za aina fulani ili kutoa vivutio vya uwekezaji. Misamaha mingine hutolewa kwa sababu za kisiasa au kijamii. Vivutio hivyo hutoa nafuu kwa kulipa kodi fulani, kwa kawaida kodi ya mapato, kodi ya zuio, kodi ya ongezeko la thamani(VAT) na ushuru wa forodha.