lengo kubwa la Serikali ya kipindi hicho ilikuwa ni kufanya wajasiliamali mitaji yao ikue na hatimae kupanua wigo wa walipa kodi, ni kama ambavyo tumeona sasa hivi Mh. Raisi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ameamua kusema nae kwamba watu wanao anza biashara hasa wenye mitaji midogo wasilipe kodi kwa mwaka mmoja, lengo ni kutaka mitaji yao ikue na hatimae serikali iweze kukusanya kikubwa hapo baadae kutoka kwa wafanya biashara hao.