Ardhi yaweza kupangishwa ama kukodishwa kwa kipindi maalum, ilimradi muda ambao mpangaji atapewa uwe pungufu ya muda ambao mwenye ardhi ana haki ya kutumia ardhi husika. Kwa mfano, kama mwenye ardhi ana hati ya miaka 99 mkataba wa kupangisha ama kukodisha ardhi hiyo utapaswa kuwa wa kipindi ambacho ni pungufu ya miaka hiyo