Kama Shahidi ataitwa na mahakama kwa lengo la kutoa ushahidi ila akakataa kutoa ushahidi au kuapishwa kutoa ushahidi mbele ya mahakama basi italazimu kesi kusimamishwa kwa muda usiozidi siku nane na katika wakati wote huo Shahidi huyo anapaswa kuwekwa kizuizini mpaka pale atakapoamua vinginevyo.