Mara nyingi ushahidi wa kusikia haukubaliki mahakamani kama, kuna ushahidi mwingine (bora zaidi) juu ya jambo hilo, shahidi hakuapishwa kabla ya kutoa ushahidi huo na shahidi hakupitia mtihani tambuka (hakuhojiwa kwa kina) na pande zote juu ya ushahidi anaoutoa.